buchspektrum Internet-Buchhandlung

Neuerscheinungen 2018

Stand: 2020-02-01
Schnellsuche
ISBN/Stichwort/Autor
Herderstraße 10
10625 Berlin
Tel.: 030 315 714 16
Fax 030 315 714 14
info@buchspektrum.de

Shadrack Nyagah

Athari za Lugha ya Kimeru katika Kazi Andishi za Kiswahili


2018. 100 S. 220 mm
Verlag/Jahr: GLOBEEDIT 2018
ISBN: 6-13-824400-1 (6138244001)
Neue ISBN: 978-6-13-824400-4 (9786138244004)

Preis und Lieferzeit: Bitte klicken


Matokeo ya utafiti huu yanalenga kurutubisha jinsi ufundishaji wa lugha ya pili hutekelezwa. Hiki ni kitabu chenye manufaa tele kwa walimu, wakuza mitaala, watafiti na wapenzi wa lugha ya Kiswahili. Wataalamu wa Kiswahili watafaidika kutokana na data nyingi iliyokusanywa nyanjani, data ambayo inaweza kutumika katika tafiti nyingine. Lugha ya Kimeru vilevile ni lugha ambayo haijaandikiwa sana kwa hivyo utafiti huu unaitendea haki kando na kuwafungulia watafiti milango ya kuitafitia lugha hii zaidi. Walimu nao, watapata fursa ya kufahamu sehemu katika lugha ambazo huwatatiza wanafunzi. Pia, watafaidika kutokana na mikakati mbalimbali ya kukabiliana na makosa haya ambayo imeshapendekezwa. Fauka ya hayo, suala la jinsia na elimu limeweza kuangaziwa. Kimsingi, hiki ni kitabu cha kila mwenye ari na ilhamu kuhusiana na masuala ya lugha.
Nyagah, Shadrack
Shadrack Nyagah ni mtaalamu wa lugha ya Kiswahili mwenye tajriba pana. Kwa sasa, anashughulikia shahada yake ya uzamifu (PHD) katika Chuo Kikuu cha Nairobi ambako anafundisha. Fauka ya hayo, amesomea Chuo cha Humboldt, Berlin. Aidha, amechapisha makala mbalimbali kwenye majarida na kuandika vitabu vya marudio. Pia, huhariri na kutafsiri makala.